Dear All!
Heri ya sikukuu ya Chismasi na Mwaka mpya, ni matumaini yangu wote muwazima wa afya njema. Msimu mpya wa shindano la Maisha Plus umekwisha shika hatamu, baada ya kumalizika kwa vipindi vya usaili na kila mkoa kujipatia washindi sasa hatua ya mwisho ya shindano hilo imefikia hatua ya kuelekea kijijini.
Lakini kuelekea katika tukio hilo la kihistoria, Disemba 31 saa tano kamili asubuhi kutakuwa na mkutano wa waandishi wa habari na washiriki 42 waliofanikiwa kuingia katika hatua hii kubwa.Mkutano huu utafanyika katika hoteli ya City Style iliyopo Sinza.
Kila mwandishi aliyetumiwa mwaliko huu athibitishe ushiriki wake kabla ya tarehe 30 saa kumi jioni. kwa njia ya barua pepe au simu na aandike namba yake ya simu.
Maisha Plus (Where Life Makes Sense)
Regards
Mratibu Habari
0717 551355
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Dec. 30, 2009

Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Dec. 5, 2009

Comments (1) posted by MUSTAPHA SELEMANI Dec. 2, 2009
Hemed ambaye huimba mahadhi ya RnB, anajipanga kuachia albam yake mchizi pia amenicha kuwa hajashirikisha msanii yoyote. Na sababu ya yeye kufanya hivyo ni kwambaa jamaa anataka kuleta utofauti katika muziki huu wa Bongo Flava. Mzigo utakuwa unaitwa "KING WA MELODY'S sooo....!!!!!! acha tuone yaliyomo yamo....??????
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Nov. 28, 2009

Kama unavyo juwa mwanzoni kulikuwa na utata kati ya Kallage na Matonya kuhusu maswala ya kazi kama unavyo juwa Kallage ni mtayarishaji wa video hapa bongo na Matonya ni msanii wa muziki wa kizazi kipya kwa maana hiyo hawa jamaa kazi zao zinategemeana hapo ndipo utata ulipoanza na ilifikia hatuwa walikuwa wanaishi kma paka na panya. Lakini kwa sasa utata wote kushinei jamaa wameelewana wapo poa sana na katika kuthibitisha hilo kesho tarehe 27 Matonya atafanya video yake ya wimbo wa MARIAM na mchizi Kallage. Lakini kwa mujibu wa Kallage mwenyewe amesema anataka kumalizana na wale wote aliowakwanza mwanzoni akiwamo Lady Jay Dee.
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Nov. 28, 2009
Its my pleasure to inform all BongoFlava, CPWAA's fans and local muisc supporters that i will have an exclusive pre-launching party on 8th Dec 2009 at Movenpic. Shughuli nzima itaanza na wageni waalikwa (V.I.P) kuanzia saa 2 usiku mpaka 5 usiku na baadae kwa kiingilio cha 15,000 TSH kwa yeyote atayependa kuingia. Usiku huo kutakuwa na uzinduzi wa tovuti zangu 2, mavazi,documentary fupi, nyimbo mpya na video zake bila kusahau Album Preview na perfomance moja ya ukweliiiiii!
Na baada ya hapo, ngoma zote za ukweli zitapigwa na maDJ wakali kutoka jijini Dar, na shangwe hilo litaendelea mpaka kuchwele. looking forward to see you there.
Support local talents, support our music! na tutafika tu.

Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Nov. 25, 2009
Shindano la Maisha Plus linafikia tamati Jumapili, ambapo mshindi ataondoka na kitita cha shilingi milioni 10 papo hapo baada kudumu kwa siku 56.
Shindano hilo lililoanza Machi 1,2009 linafikia tamati ikiwa ni sehemu ya kwanza na ya pekee katika historia ya mashindano ya uhalisia( Reality Shows) nchini Tanzania.
Mratibu wa shindano hilo, David Sevuri anasema shindano hilo linamalizika huku malengo yakiwa yamefikiwa kwa kiasi kikubwa.
“Tulilenga kuwawezesha vijana kujitambua,Kuwapa ujuzi kwa kuwafundisha vitu mbalimbali, Kuendeleza vipaji vyao,kuwapa mtazamo chanya wa maisha watazamaji na washiriki,kubadilishana utamaduni na kuburudisha watazamaji, tunajivunia kusema kuwa tumeweza kufanikisha yote haya” alisema.
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 22, 2009

Comments (1) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 22, 2009
Miloni kumi imetengengwa kwa mshindi lakini uamuzi wa kumpa mshindi upo kwa mashabiki ambao ndio waamuzi katika shindano hili.
Maulid 33, Hamis 15, Moshy 19, Abdul 32, Charles 11
Steve 14, Upendo 18, Boniface 20, Teddy 36 Modesta 37
Unaweza kupiga kura kwenye mtandao ambao ni maishaplus.g5click.com au kwa njia ya simu kwenda 15522.
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 22, 2009
Ni miezi miwili imepita tangu shindano hilo lianze, kutokana na uhalisia wa shindano hilo kureflect maisha ya Watanzania wengi wameomba liendelee kuwepo,kwa mujibu wa waandaaji shindano hilo litarejea baada ya mapumziko ya muda mfupi.
Mraribu wa shindano hilo David Sevuri ameliambia Starehe kuwa kutokana na maoni ya watu wengi shindano hilo litakuwa tena TBC1 baada ya timu ya shindano hilo kijipanga upya.
“Tutarudi tena tukiwa tumeliboresha zaidi shindano hili, lakini watazamaji bado watakuwa na vitu vingi vya kutazama kwa wakati wote ambao hatutakuwepo kijijini kwa kuwa tuna vitu vingi havijaonyeshwa” alisema.
Sevuri alisema kipindi cha Maisha Plus cha Jumapili kitaendelea kama kawaida kwa muda wote wakati ‘season’ II ikisubiriwa.
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 22, 2009


Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 19, 2009

Comments (3) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 14, 2009
Mkoa wa Mwanza ndio mkoa pekee unaowakilishwa na washiriki wote watatu mpaka katika hatua ya fainali huku mikoa mingine kama Tanga ikiwa imepoteza washiriki wake mapema.
Mwanza inawakilishwa na Moshy Mahona, Boniface Michael na Upendo Peneza ambaye ndiye pekee aliyewahi kuingia kiaangoni huku wengine wakiendelea 'kutesa'.
Mikoa ambayo imepoteza washiriki wake wote ni Tanga, Dodoma na Mbeya.
Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 14, 2009

Comments (0) posted by MUSTAPHA SELEMANI Apr. 14, 2009
Automotive (3)
Entertainment (4)
General (32)
Government (0)
Maisha Plus (32)
Mimi Ni Kisura (0)
News (0)
Shopping (0)
Sports (0)
Welcome to
G5 world
G5 CLICK ENT. COMPANY ©2009 | About Us | Youtube | Official BLOG
![]() |
