Kwa miaka mingi tumeshuhudia wanamuziki wa muziki wa dansi wanapokuwa katika band mojawapo wanafanya vizuri, wakisha pata jina hupata tamaa aidha ya kuhama band au kuanzisha band zao kwa matumaini kwamba kipato kitaongezeka. Lakini kinyume na matarajio yao hali inakuwa tofauti, matokeo yake wanakuwa hawavumi kama walipokuwa katika band zilizo ibua vipaji vyao. Mfano mzuri ni kwa wanamuziki kama Ali Choki, Banza Stone , Muumin Mwijuma na wangineo wameshuka sana kimuziki, ndo tuseme wamesha vichakachua vipaji vyao kwa kuhamahama, naomba wadau mnisaidie.